Jumapili, 12 Februari 2017

LIVE KUTOKA COMORO: NGAYA 1 VS 5 YANGA (FULL TIME) MPIRA UMEKISHAAAA Dk 89, Yanga wanaendelea kushambulia kwa kasi, Chirwa anaingia lakini Mohamed Zahir anamzuia hapa Dk 88, Makapu anafanya kazi ya ziada kuukoa mpira kutoka kwa Said aliyekuwa ameingia vizuri Dk 87, Zulu tena, anajaribu shuti la mbali na mpira unaokolewa na mabeki wa Ngaya Dk 84 Yanga wanaingia vizuri, pasi ya Kamusoko, Chirwa anajaribu inawababatiza mabeki wanaokoa Dk 80, Ngaya wanaingia tena kwenye lango la Yanga lakini Dida anadaka na mwamuzi anasema ni faulo. Juma Abdul anaonekana kuumizwa, anatibiwa hapa SUB Dk 78 anaingia Said Juma Makapu kuchukua nafasi ya Simon MSuva. Hii inaonekana Lwandamina ameamua kuimarisha kiungo zaidi baada ya kuona Ngaya wanacheza katikati Chirwa anaingia vizuri tena Dk 76, Ngaya wanaonekana kuamka na kucheza vizuri katikati lakini bado mashambulizi yao si makali GOOOOOOOO Dk 73, Kakumusoko anaachia mkwaju mkali kwelikweli unajaa wavuni ilikuwa ni baada ya kupokea pasi ya Niyonzima Dk 70, Yanga wanaendelea kushambulia kwa kasi na Ngaya wanalazimika kuwa makini lasivyo watakutana na mvua ya mabao GOOOOOOO Dk 66 Said Khalfan anaachia Mkwaju mkali na kuandika bao kwa Ngaya GOOOOOOO Dk 65, Tambwe anaunganisha krosi safi ya Juma Abdul na kuandika bao la nne (Mashabiki wa Ngaya wanaanza kuondoka uwanjani) GOOOOOOOOO Dk 59, Kamusoko anamchambua kipa na kutoa pasi safi kwa Chirwa ambaye anaandika bao saaafi kabisa Dk 57 kona safi ya Said, mpira unamkuta Juma Abdul, inakuwa kona tena, inachongwa mara ya tatu Cannavaro anaondosha hapa Dk 56, Alfa anaingia na kupiga mpira krosi hapa lakini Dida anapangua na kuwa kona, inachongwa tena na kuwa kona tena SUB Dk 56 Nyanga wafanya mabadiliko tena, Ali anatoka na nafasi yake inachukuliwa Derita Alfa Dk 55, kuna wachezaji wanaingia kumbeba mchezaji aliyeumia wa Ngaya. KADI Dk 50, Saidi wa Ngaya analambwa kadi ya njano kwa kumfanyia madhambi Kamusoko aliyekuwa ameishamtoka SUB Dk 48 Ngaya wanafanya mabadiliko Said Haligan anaingia kuchukua nafasi ya Azeraden Dk 47, Msuva anaingia vizuri tena hapa, anaachia mkwaju mkali hapa lakini Ngaya wako makini Dk 45 Mpira umeanza, Yanga wanaanza kwa kasi na Msuva anaingia na kuachia mkwaju lakini Goal kick MAPUMZIKO Dk 45+2 nafasi nyingine kwa Yanga, kipa akiwa nje ya lango lakini Tambwe anashindwa kulenga na kuwa goal kick GOOOOOOOOO Dk 45+1, Msuva anaachia mkwaju mkali kutoka pembeni na kuandika bao la pili kwa Yanga Dk 45, Msuva anaingia vizuri anagongeana na Niyonzima anaachia mkwaju mkali lakini kipa Said Komandoo anaruka na kudaka kama nyani hapa Dk 44, Tambwe anakwenda vizuri hapa anawekawa chini hapa. Faulo inachongwa na Chirwa lakini Said Komandoo anaudaka kwa mbwembwe hapa GOOOOOOOOOOOOOO Dk 43, Haji Mwinyi anapiga mpira wa mrefu, Chirwa anauwahi na kupiga pasi safi kwa Zulu ambaye anaachia mkwaju saafi na kuandika bao moja kwa Yanga Dk 42, hatari kabisa katika lango la Yanga, Dida anaruka kuupiga ngumi mpira, lakini hakuupiga kwa nguvu, ukatua kwa Al Manana, naye akaachia shuti ambalo licha ya kutokuwepo kwa kipa lakini hakulenga lango Dk 40, krosi nyingine nzuri ya Mwingi, Tambwe anaruka hapa lakini kila Said Komando anaruka na kuudaka vizuri kabisa Dk 36, Yanga wanaonekana kuwa wepesi na wanapeleka krosi nyingi zaidi lakini mara nyingi kunakuwa hakuna watu wa kuzitumia. Lakini inaonekana hata mabeki wa pembeni wakati wanataka kufunga wao, jambo ambalo linawakosesha nafasi za kufungaDK 35, Yanga wanapata kona nyingine, inachongwa na Niyonzima lakini wanaokoa Ngaya na kuwa wa kurushwa Dk 31, Tambwe katika nafasi nzuri baada ya kupokea pasi nzuri ya Chirwa, yeye na kipa wa Ngaya aitwaye Komando. Lakini Tambwe anapaishaa juuuu Dk 30 hatari kwenye lango la Yanga, Fadhul wa Ngaya anaingia vizuri na kuachia mkwaju mkali lakini Dida yuko imara Dk 29, Niyonzima anachonga kona safi, inaondoshwa. Mpira unamkuta Juma Abdul na kuurudisha kwa Niyonzima na anaachia shuti kali lakini hakulenga Dk 28, Yanga wanapata kona ya kwanza baada ya krosi safi ya Zulu kuokolewa Dk 24, Dida anaonyesha umahiri kwa kuuwahi mpira baada ya Cannavaro kuteleza na kuanguka Dk 18, mpira wa Haji Mwinyi unakwenda juujuu na kugonga mwamba na kutoka nje. Goal kick Dk 16, krosi nzuri ya Juma Abdul ilitua langoni mwa Yanga lakini mwamuzi amesema ni madhambi Hata hivyo, Yanga wamekuwa wakijibu mashambulizi hayo kwa mipira ya krosi Mechi imeanza kwa kasi na Ngaya wamekuwa wakishambulia sana KIKOSI CHA YANGA 1. Deogratius Munishi 2. Juma Abdul 3. Mwinyi Haji 4. Nadir Haroub 5. Kelvin Yondani 6. Justin Zullu 7. Saimoni Msuva 8. Thabani Kamusoko 9. Amisi Tambwe 10. Obrey Chirwa 11. Haruna Niyonzima Akiba - Ali Mustafa - Hassani Kessy - Oscar Joshua - Emanuel Martin - Juma Mahadhi - Juma Saidi - Deusi Kaseke

Jumamosi, 11 Februari 2017

LIVE KUTOKA UWANJA WA TAIFA: SIMBA 3 VS 0 PRISONS (KIPINDI CHA PILI) SUB Dk 74 Pastory Athanas anaingia kuchukua nafasi ya Ibrahim Ajib Dk 73, Prisons wanaingia vizuri na Meshack anauchonga vizuri mpira lakini unatoka nje kidogo mwa lango la Simba Dk 73, pasi nzuri ya Mavugo, Kazimoto anaachia shuti kali hapa, lakini kipa anadaka Dk 72, Ndemla anaachia shuti kali hapa lakini goal kick SUB Dk 70 Shiza Kichuya anaingia kuchukua nafasi ya Liuzio GOOOOOOO Dk 68, Mavugo anaifungia Simba bao la tatu kwa Kichwa akiunganisha krosi ya outer ya Ajibu Dk 65 Chona wa Prisons naye yuko chini paleSUB Dk 62, Kazimoto anaingia kuchukua nafasi ya Mwanjale Dk 62 Mwanjale anatolewa nje kwenda kutibiwa Dk 61, Mwanjale yuko chini baada ya kuumia, inaonekana hataendelea kwani mara ya pili ndani ya dakika 5 anaanguka na kutibiwa Dk 58, Agyei tena anaikoa Simba baada ya krosi dongo ya Kimenya Dk 57, Krosi ya Bukungu ndani ya eneo la hatari lakini haikumfikia yoyote, Prisons wanaokoa SUB Dk 56 upande wa Prisons Meshack Selemani anaingia kuchukua nafasi ya Benjamin Asukile Dk 55, Mavugo anawatoka mabeki wa Simba, wanaokoa na kuwa kona, inachongwa lakini goal kick Dk 54, Prisons wanaingia ndani ya eneo la hatari la Simba, Agyei anafanya kazi ya ziada tena Dk 51, krosi nzuri ya Kimenya ndani ya lango la Simba, Agyei anatokea na kudaka kama nyani Dk 49, Hamisi wa Prisons anageuka vizuri na kuachia mkwaju lakini unakuwa goal kick Dk 47, Mwanjale anafanya kazi ya ziada kuokoa mbele ya Asukile aliyekuwa anakwenda kumuona Agyei, yuko chini anatibiwa sasa Dk 45, kipindi cha pili kimeanza na kila upande unaonekana kuwa makini

Jumatano, 8 Februari 2017

Antonio Conte : “Naweza kuua mtu” Mzuka wa kocha Antonio Conte anapokuwa uwanjani umekuwa kivutio sana kwa mashabiki wa soka.Conte amekuwa mwenye furaha sana pale Chelsea inapopata ushindi haswa dhidi ya timu ngumu.Conte amekuwa akifanya mambo yanayowashangaza watu wengi kutokana na mizuka yake uwanjani mfano tukio alilofanya juzi alipoonekana kama anampiga kofi kocha wake msaidizi akimuelekeza kitu. Antonio Conte amekiri kwamba kocha wake msaidizi Angello Allesio amekuwa mhanga mkubwa wa mizuka yake.Allesio ndio mtu anayekaa pembeni na Conte na hii inamfanya kukumbana na dhahma zote za Muitaliano huyo anapopandisha mizuka.Hali hii huwashangaza watu wengi lakini Allesio anaonekana kumzoea Conte. Conte amekiri kwamba anaweza hata kuua mtu,Conte amesema akiona kitu hakiendi sawa huwa anachanganyikiwa sana “nikiona jambo halipo sawa,naweza kufanya lolote nadhani naweza hata kuua mtu” Conte aliiambia Sky Sports.Conte alisema katika mechi ya Arsenal alimuona Kante amekaa sehemu isiyo sahihi na alitaka kumuelekeza ila akamuona Allesio yuko pembeni ndipo alimpiga yeye akimuambia amuelekeze Kante. Conte anadai aliamini sana mbinu zake wakati anakuja Uingereza japo mechi za kwanza la ligi hiyo walishinda lakini hakuona kama walishinda kwa kutumia mbinu zake.Conte anasema anashukuru kuona mbinu zake zikiitoa Chelsea chini na sasa kuwa kati ya timu za kuogopwa nchini Uingereza. Lakini Conte bado haamini kwamba Chelsea itakuwa bingwa,Conte anasema ligi ya Uingereza hakuna kitu kiitwacho “mechi rahisi” na amewataka vijana wake wapambane tu hadi mwisho.Conte ametolea mfano Liverpool walivyofungwa na Hull City huku akikiri kwamba angependa mechi kati ya Swansea na Man City ingeisha suluhu.

MANJI AAMUA KWENDA SENTRO POLISI KESHO BADALA YA IJUMAA, ATAKA YEYE NA MAKONDA WAPIMWE Mwenyekiti wa Yanga, Yusuf Manji kesho amepanga kwenda kuripoti Kituo Kikuu cha Polisi cha jijini Dar es Salaam maarufu kama "Sentro" kesho badala ya keshokutwa . Manji ameyasema hayo hivi punde saa chache tangu Mkuu wa Mkoa wa Polisi wa Dar es Salaam , Paul Makonda kutangaza majina 65 ya wanaitakiwa kufika kwenye kituo cha hicho kikubwa cha Polisi ili kusaidia vita ya kupambana na madawa ya kulevya kama sehemu ya wanaotumihumiwa au la. Akizungumza na Waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam, Manji alisema kuwa hawezi kubadili ratiba zake keshokutwa na kwenda kupanga foleni ya watu 65 kwa ajili ya kitu hicho. Manji alisema, ana kazi nyingi za kufanya hiyo keshokutwa ijumaa, hivyo ataenda kesho asubuhi na mapema sana ili kutekeleza suala hilo aliloitiwa. Pamoja na kukubali kwenda tena mapema, Manji amesema amepanga kuchukua hatua za kisheria kwa kwenda mahamakani kwa ajili ya kumfungulia mashtaka Makonda. "Mimi nitaenda kituo cha Polisi kesho asubuhi na mapema na sisubiri hiyo Ijumaa anayotaka yeye Makonda naomba nieleweke. "Baada ya kutoa huo ushirikiano Polisi, basi nitaenda mahakamani kumfungilia mashtaka Makonda kwa kunidhalilisha kwa kutumia vibaya jina langu, kwani kitendo cha kutumia jina la mtu vibaya ni makosa na katiba ya nchi inaniruhusu kumshtaki Makonda," alisema Manji. "Kama kweli mtu unamuita kukusaidia kwa ajili ya madawa ya kulevya, vipi unamtangaza mbele ya hadhara. Akishakutajia utaweza vipi kumlinda muda wote, ingekuwa vizuri kumuita kimyakimya, halafu akutajie na wewe ufanyie kazi hasa kama uliona anajua," alisema. "Kweli nitakwenda Alhamisi, niko tayari kupimwa na kusachiwa. Lakini ningependa na Makonda apimwe pia na kusachiwa. "Sikatai kuwepo na vita ya madawa, lakini hauwezi ukafanya kila kitu bila ya kujali haki za watu, heshima zao, majina yao. Hii si sawa na siwezi kukubali."

LIVE KUTOKA MAJIMAJI SONGEA: MAJIMAJI 0-2 SIMBA GOOOOOOOOO Dk 64 Ndemla anaachia mkwaju mkali na kuiandikia Simba bao la pili. Ulikuwa ni mpira safi wa kona, Majimaji wakajichanganya naye hakufanya ajizi Dk 63, Simba wanagongeana vizuri, Mavugo anampa Kotei anaachia shuti kali, linaokolewa na kuwa kona SUB DK 60, James Kotei anaingia kuchukua nafasi ya Ajibu, mfungaji wa bao pekee hadi sasa Dk 58, Mavugo anamchambua beki hapa, anaachia mkwaju lakini hakulenga langoDk 57 sasa, Majimaji ndiyo wanaoshambulia sana, Simba wanapaswa kuwa makini kwa kuwa inaweza kuwa hatari kwao Dk 56, Kaheza, yeye na kipa anapiga lakini mpira wake unamgonga kipa na kwenda nje. Kona, inachongwa lakini haina faisa DK 52, mpira mzuri wa Mavugo unaokolewa na kuwa kona, inachongwa na kuzaa kona nyingine SUB Dk 52, Simba wanamtoa Juma Liuzio na nafasi yake inachukuliwa na Pastory Athanas Dk 50, Sabato anajaribu kumtoka Mwanjale lakini anautoa na kuwa kona, inachongwa, Agyei anapangua na mabeki wanaondosha Dk 49, Kibuta anageuka na kuachia mkwaju mkali kwa mara nyingine, lakini hakulenga lango. Goal kick Dk 47 Simba wanagongeana vizuri kabisa hapa na Ajibu anaachia mkwaju mkali kabisa lakini sentimeta chache, goal kick Dk 45, mechi imeanza kwa kasi na Simba wanakuwa wa kwanza kufika kwenye lango la Majimaji MAPUMZIKO Dk 45+1 shuti la mpira wa adhabu wa Kaheza, Agyei anatema na mabeki wake wanaokoa. Inakuwa kona lakini haina manufaa kwa Majimaji DK 45+1, krosi nzuri kabisa, Kibuta yeye na kipa wa Simba, anafumba macho na kuukosa mpira DAKIKA 1 YA NYONGEZA Dk 45, Majimaji wanaingia tena kwenye lango la Simba lakini Mwanjale anaokoa mbali kabisa DK 44, nafasi nzuri kwa Majimaji, Sabato anaupata vizuri anapiga kichwa lakini anashindwa kulenga DK 42 sasa, Majimaji wanaonekana kufunguka na kucheza vizuri lakini hawako makini sana wanapoingia kwenye lango la Simba Dk 40, Kipangile wa Majimaji anaingia kwenye lango la Simba, lakini anashindwa kutulia Dk 39, Selemani Kibuta mbele ya Muzamiru anaachia mkwaju mkali kabisa hapa, unatoka pembeni kidogo ya lango la Simba Dk 35, Mavugo anapokea pasi nzuri ya Ajibu na kupiga shuti kali, linatoka sentimeta chache kabisa Dk 31, Sabato anaingia vizuri tena na kuachia shuti lakini hakulenga Dk 28 Majimaji wanapoteza nafasu nzuri hapa na Agyei anadaka vizuri kabisa Dk 22, Sabato anapoteza nafasi nzuri baada ya kuunganisha kichwa karibu na lango la Majimaji lakini hakulenga GOOOOOOO Dk 19, krosi safi ya Shiza Kichuya, Ajibu anaunganisha vizuri kwa kichwa na kuandika bao la kwanza kwa Simba Dk 15 sasa, Simba wanaonekana na kugongeana vizuri lakini bado hakuna kashkash kubwa wanayofikisha langoni Dk 12, Kona ya pili wanapata Majimaji hapa baada ya Bukungu kuutoa mpira nje, inachongwa lakini Agyei anadaka Dk 11 Simba wanagongeana vizuri na Liuzio anaupachika mpira wavuni. Mwamuzi anasema kabla, tayari alikuwa ameotea DK 9, krosi inapigwa langoni mwa Simba, kipa Agyei anakwenda markiti lakini Zimbwe au Tshabalala anajitokeza na kuokoa vizuri kabisa Dk 8, kona ya kwanza ya mchezo wanapata Majimaji baada ya Mwanjale kuutoa mpira kwa kichwa Dk 7, Peter anageuka na kuachia mkwaju hapa lakini Agyei anadaka kwa ulaini Dk 7 sasa, bado mpira unachezwa zaidi katikati ya uwanja na hakuna mashambulizi makubwa ndani ya Dk 2 Simba wanaingia kwenye lango la Majimaji, Mazamiru anapiga shuti linawababatiza mabeki hapa na wanaokoa Dk ya 1, Majimaji wanaanza kwa kasi, krosi nzuri inapigwa hapa lakini mwamuzi anasema offside KIKOSI CHA SIMBA: 1. Daniel Agyei 2. Janvier Bukungu 3. Mohamed Zimbwe 4. Novatus Lufunga 5. Method Mwanjale (C) 6. Muzamiru Yassin 7. Shiza Kichuya 8. Said Ndemla 9. Laudit Mavugo 10. Juma Liuzio 11. Ibrahim Ajibu SUB Peter Manyika Mwinyi Mazimoto James Kotei Haji Ugando Athanas Kitandu 04 Feb 2017