LIVE KUTOKA UWANJA WA UHURU: RUVU SHOOTING VS SIMBA (MAPUMZIKO) MAPUMZIKO
GOOOOOOOOO, Mpira wa krosi safi, Mo Ibrahim anaunganisha kwa shuti kali kabisa hapa
-Kona safi inachongwa hapa, Banda anajitishwa vizuri hapa. Goal kick
-Simba wanaingia vizuri kabisa, Zimbwe anapiga krosi lakini Makwaya anaokoa, konaaa
DAKIKA 3 ZA NYONGEZA
Dk 45 sasa, mpira mwingi unachezwa katikati zaidi
Dk 43, nafasi nyingine kwa Simba, MZamiru anauwahi mpira ukizagaa anaachia shuti kali lakini unapita juuuu
KADI Dk 41, kipa Bidii Hussuein analambwa kadi ya njano kwa kupoteza muda
Dk 40, Simba wanapoteza nafasi nyingine ya wazi, Pastory anashindwa kulenga
KADI Dk 38, Jabir Aziz Stima analambwa kadi ya njano kwa kumrushia daruga Athanas
Dk 36, mkwaju wa adhabu wa Abdi Banda unapigwa na kupaa juu ya lango
DK 32, Zimbwe anaingia vizuri lakini JKT wanakuwa wepesi kuokoa
Dk 29, Shooting wanafanya shambulizi kali hapa, kona. Hii ni kona ya kwanza ya Ruvu leo
Dk 26, Mo Ibarahim anaachia mkwaju mkali lakini Juhudi anadaka kwa ustadi mkubwa hapa
Dk 20, Ruvu wanaonekana kuwa na kasi zaidi na kuanza ksuhambulia kwa kasi zaidi
DK 14, krosi safi, mpira unapigwa na kugonga mwamba. Lakini sasa kipa wa Ruvu yuko chini akitibiwa
Dk 13, Mo Ibra anaingia vizuri hapa ndani ya 18, Ruvu wanaokoa na kuwa konaaaaa
Dk 11, mpira umesimama hapa Kisiga akiwa anatibiwa hapa
Dk 9, Simba wanafanya shambulizi la haraka, Mwanjale anapanda akigongeana na wenzake, anatoa krosi safi kwa Pastory, yeye na nyavu anapaishaa buuuuu
Dk 6, Simba wanaendelea kulisakama lango la Ruvu, Mo Ibra anaingia vizuri na kupiga shuti kali, kipa anadaka mpira unamtoka lakini anawahi
Dk 4, krosi nzuri ya Kichuya, Athanas anaunganisha tena, lakini Shooting wanaokoa
Dk 2, krosi safi ya Zimbwe, Athanas anapiga kichwa hapa lakini ni goal kick
Dk 1, Simba wanaanza kwa kasi wakionekana wamepania kupata bao
KIKOSI CHA SIMBA
1. Daniel Agyei
2. Besaka Bukungu
3. Mohammed Hussein
4. Abdi Banda
5. Method Mwanjale
6. Jonas Mkude
7. Shiza Kichuya
8. James Kotei
9. Pastory Athanas
10.Muzamiru Yassin
11. Mohammed Ibrahim
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni