Jumamosi, 7 Januari 2017

ROONEY AIKAMATA REKODI YA SIR BOBBY CHARLTON MAN UNITED IKIUA 4-0 FA Mshambuliaji Wayne Rooney akishangilia baada ya kufunga bao lake la 249 Manchester United na kuifikia rekodi ya gwiji Sir Bobby Charlton aliyekuwa anaongoza kwa kuwafungia mabao mengi Mashetrani hao Wekundu. Rooney alifunga bao hilo dakika ya saba katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Reading kwenye mchezo wa Raundi ya Tatu Kombe la FA England Uwanja wa Old Trafford. Mabao mengine ya United yamefungwa na Anthony Martial dakika ya 15 na Marcus Rashford mawili dakika za 75 na 78

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni