pata dondoo mbalimbali za michezo ya ndani na nje ya nchi.mompondazy itakujuza kila kitu.
Jumanne, 3 Januari 2017
Ushindi mwingine umeiongezea Simba pointi Mapinduzi Cup 2017 Simba imefikisha pointi 6 baada ya kupata ushindi wa goli 1-0 mbele ya KVZ kwenye mchezo wao wa pili wa Kundi A michuano ya Mapinduzi Cup 2017. Bao pekee la ushindi wa Simba limefungwa na kiungo Mzamiru Yassin dakika ya 44 kipindi cha kwanza ambalo lilidumu kwa muda wote uliosalia. Simba wamepata ushindi wa pili mfululizo baada ya kushinda 2-1 kwenye mechi yao ya kwanza dhidi ya Taifa Jang’ombe wakati KVZ wao wamepoteza mechi zao mbili na kujiweka kwenye nafasi finyu ya kusonga mbele. Ratiba ya leo Jumatano January 4, 2017 Kundi B Saa 10:00 jioni Yanga vs Zimamoto Saa 2:15 usiku Jamhuri vs Azam
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni