Jumapili, 23 Oktoba 2016

HAMILTON ASHINDA US GRAND PRIX Dereva Lewis Hamilton amefanikiwa kushinda US Grand Prix huku dereva mwenzake wa Mercedes Nico Rosberg akishika namba 2 na Daniel Ricciardo wa Red Bull akishika namba 3. Bingwa huyo mtetezi Sasa ameshinda Grand Prix 50 tangu aanze kushiriki katika michuano ya Formular 1 na hii ni mara ya 3 mfululizo anashinda mbio hizi za Marekani Ushindi huu unamfanya Hamilton kuwa nyuma ya Rosberg kwa pointi 26 katika msimamo wa madereva huku zikiwa zimebaki mbio 3 msimu kumalizika. #F1

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni