pata dondoo mbalimbali za michezo ya ndani na nje ya nchi.mompondazy itakujuza kila kitu.
Jumatano, 4 Januari 2017
AZAM FC YAAMBULIA SULUHU KWA JAMHURI, BOCCO AIZUNGUMZIA YANGA, ASEMA KAZI IPO Azam FC inalazimika kuisunga Yanga ili kufuzu katika hatua ya mtoano ya Kombe la Mpinduzi. Hiyo inatokana na matokeo ya mchezo wao wa leo baada ya kupata sare ya bila mabao dhidi ya Jamhuri kwenye Uwanja wa Amaan mjini Zanzibar, leo usiku. Hata hivyo, John Bocco ambaye ni nahodha wa Azam FC, amesema kazi ni ngumu kwa kuwa Yanga ni timu kubwa. “Tunawaheshimu Yanga kwa kuwa ni timu kubwa. Tunajua nasi ni timu kubwa na bora, itakuwa mechi ngumu sana. “Lakini tunaiweka kando mechi ya leo na tunaanza maandalizi kwa ajili ya mechi ijayo kujiandaa dhidi ya Yanga,” alisema. Kabla ya kukutana na Azam FC leo, Jamhuri ilikuwa imekutana na dhoruba ya kipigo cha mabao sita kutoka kwa Yanga.
Jisajili kwenye:
Chapisha Maoni (Atom)
Hakuna maoni:
Chapisha Maoni